
Mgombea urais wa DP kutoa matibabu, chakula bure kwa wanawake na watoto
Mgombea urais kupitia Chama cha Democratic Party (DP), Abdul Mluya, ameahidi kuwa endapo atapata ridhaa ya kuingia madarakani, serikali yake itahakikisha wanawake, watoto, wazee na watu wenye ulemavu wanapata matibabu bure huku akinadi mpango wa kuwapatia chakula bure wanawake wanaotoka kujifungua ndani ya miezi mitatu ya kwanza.